Hatimaye Tundu Lissu Apewa Dhamana
Hatimaye Tundu Lissu Apewa Dhamana
Mbunge wa Singida Mashariki Tundu Lissu amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akikabiliwa na mashtaka manne ya uchochezi.
Wakili wa Serikali Kishenyi Mutalemwa aliwasilisha maombi ya kupinga dhamana yaTundu Lissu kwa madai kwamba amekuwa na mwenendo unaohatarisha amani si tu kwa wanajamii, bali hata kwake mwenyewe kwa kuendelea kutoa maneno ya uchochezi.
Hakimu Huruma Shaidi, ametupilia mbali ombi hilo la serikali na
kumpa Tundu Lissu dhamana ya shilingi Milioni 20

No comments: